Posts

Royal Tour imeleta mazao lukuki ya utalii- DK Abbasi

Image
   Na John Mapepele Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii na Mwenyekiti wa Kamati ya Kuitaingaza Tanzania ya Royal Tour, Dkt. Hassan Abbasi amesema wakati Tanzania imetimiza mwaka mmoja toka Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan atoke ofisini na kucheza filamu ya Royal Tour, kumezaliwa mazao mbalimbali ya utalii hapa nchini. Dkt. Abbasi ametoa kauli hiyo leo Mei 1, 2023 wakati akihitimisha mjadala wa kitaifa kwenye mtandao (Zoom Meeting) uliojumuisha wadau mbalimbali wa utalii  duniani na  kurushwa mubashara  ya  mitandao na vyombo  mbalimbali vya habari ulioangazia mafanikio  yaliyopatikana  katika kipindi cha mwaka mmoja wa Royal Tour. Amesema kutokana shuhuda nyingi zilizotolewa na wadau kuwa  kumekuwa na mafanikio makubwa katika kipindi kifupi tangu Roal Tour ilipozinduliwa  inapaswa  kila mtanzania kuwa balozi wa  kuitangaza Tanzania ikiwa ni mkakati wa kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu...

Mhe. Mchengerwa- Serikali kuwashirikisha wadau kwenye mnyororo wa thamani wa utalii

Image
  Na John Mapepele Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema Serikali imedhamiria kufanya kazi kwa pamoja na wadau mbalimbali wa utalii nchini kwa ajili ya kuimarisha mahusiano ya serikali na wadau (Public Private Partnership) ili kufikia kwa haraka   lengo la  kuwapata  watalii  milioni tano hatimaye  kuchangia  kwenye uchumi wa nchi. Akizungumza kwenye Tamasha la Kwanza la Biashara la Wadau wa Utalii leo, Februari 23, 2023 lililopewa  jina la “The Z sumit” ambapo Rais wa Zanzibar, Mhe. Hussein Mwinyi amekuwa Mgeni Rasmi, Mhe. Mchengerwa amesisitiza kuwa  dhamira ya serikali kwa sasa ni kuwashirikisha wadau  wote  kwenye mnyororo wa thamani wa utalii ili kutoa huduma  ya kiwango cha kimataifa kitakachowavutia watalii kuja kujionea vivutio mbalimbali vya utalii hapa nchini. Aidha, amemhakikishia Mhe. Rais Mwinyi kufanya kazi kwa karibu na Waziri anayesimamia sekta ya Utalii kwa upande wa Zanzibar katik...

Serikali yawazawadia Watanzania Sports Arena siku ya valentine.

Image
  Na John Mapepele Leo ikiwa ni siku ya wapendanao duniani (valentine) Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo  imepokea kutoka Shirika la Nyumba ( NHC) eneo la ekari 12  Kawe Jijini Dar es salaam litakalojengwa Ukumbi wa Kimataifa wa kisasa wa Michezo (Sports Arena). Akizungumza na Wanahabari  mara baada ya kukabidhiwa, Waziri wa utamaduni sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa aliyeambatana na Katibu Mkuu Dkt. Hassan Abbasi amesema, Wizara inakwenda kulikabidhi eneo hilo mwezi Machi kwa Mkandarasi na ujenzi utachukua muda wa miezi 08 hadi 10  umekamilika. Aidha, Mhe. Mchengerwa ameeleza kuwa dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Dkt.Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha sekta ya burudani na michezo zinakuwa  Sekta zinazochangia kwa kiasi kikubwa kwenye pato la Taifa na wananchi wananufaika nazo Amesisitiza kuwa watanzania wana kiu ya kuona Ukumbi wa Kimataifa wa michezo kama zilivyo nchi zingine unajengwa nchini Tanzania. Amefafanua kuwa ...

TAARIFA YA UFAFANUZI KUTOKA WIZARA YA UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO

Image

WAZIRI MCHENGERWA KUPOKEA TATU KUBWA YA KIHISTORIA FEBRUARI 3,2023

Image
  ************************* WAZIRI wa Utamaduni Sanaa na Michezo Mohamed Mchengerwa anatarajiwa kupokea Mageuzi matatu ya kihistoria katika wizara hiyo siku kesho Februari 03,2023 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano Mwalimu Nyerere (JNICC) Jijini Dar es salaam. Akizungumza na Wanahabari Leo Februari 02,2023 Ofisi za Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) Katibu Mkuu wa Wizara ya Sanaa na Utamaduni Dkt.Hassan Abbas amesema Wizara hiyo siku ya kesho inaenda kuandika historia kubwa 3 zenye mchango mkubwa kwa taifa la Tanzania. "Ni lazima nchi ya Tanzania tuwe na Muziki ambao unalimtambulisha taifa hivyo tuliteua kamati ambayo iliongozwa na watu wabobezi katika kuhakikisha mdundo unapatikana kwa kuzingatia mdundo huo haupotezi vionjo vya kitamaduni ya kitanzania." Hata Katibu mkuu ameeleza kuwa Kamati hiyo ilisheheni watayarishaji mbalimbali na wadau wakubwa wa Kimuziki. "Kamati hii iliongozwa na Mwenyekiti Dkt.Kedmon Mapana nafikiri umahiri wake unafahamika ,Masoud Masoud manji ...

Mhe. Mchengerwa- Serikali yadhamiria kujenga Chuo Kikuu cha Kiswahili.

Image
  Na John Mapepele Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe Mohamed Mchengerwa amesema Serikali imedhamiria kujenga Chuo Kikuu cha Kiswahili ili kukuza na kubidhaisha  lugha hii adhimu duniani. Mhe. Mchengerwa amesema haya leo, Januari 25, 2023 jijini Dar es Salaam wakati akimkaribisha   Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa kuhutubia kwenye hafla ya utoaji wa Tuzo ya Kiswahili. Amesema, hivi sasa Kiswahili ni miongoni mwa lugha zinazokua na kuenea kwa kasi kubwa ulimwenguni ambapo Kiswahili ni miongoni mwa lugha kubwa kumi duniani. Hivyo, kasi ya ufunzaji na ujifunzaji wa lugha hii imekuwa ikiongezeka kila uchao. Aidha,  amesema Kiswahili ni lugha ya mawasiliano mapana katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na kwa upande wa Tanzania licha ya kuwa lugha ya Taifa ndiyo lugha kuu ya mawasiliano. Amefafanua kuwa  lugha ya  Kiswahili kwa sasa imevuka mawanda ya kuielezea lugha yenyewe na hivyo inatumika kuelezea taaluma mbalimbali kama vile afya,...

Mhe. Mchengerwa atatua mgogoro wa mwekezaji na wananchi, wananchi wampongeza Rais Samia.

Image
  Na John Mapepele Wananchi wa eneo la Nyanda  na Utunge wilayani Rufiji wamemshukuru Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mbunge wa Rufiji na MNEC wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Mohamed Mchengerwa kwa kutatua mgogoro wa muda mrefu baina ya mwekezaji wa mradi wa uzalishaji wa sukari na wananchi wa maeneo hayo. Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa wananchi na Mhe. Mchengerwa leo, Januari 22,2023 kwenye eneo la Nyanda, Mwenyekiti Mstaafu wa Kijiji hicho, Amir Omary Magulu amempongeza Mhe. Mchengerwa kwa busara na  jitihada  zake  za kuumaliza  mgogoro huo ambao ulikuwa sugu kwa muda mrefu sasa. Amesema mgogoro huo baina ya mwekezaji huyo ambaye ni Lake Agro  unatokana na ukiukwaji wa makubaliano ya awali  ya  kupewa eneo la uwekezaji na  kutopata taarifa sahihi za uwekezaji. Akitoa suluhisho la mgogoro hilo, Mhe. Mchengerwa ameuomba uongozi wa Wilaya na Halmashauri ya Rufiji kuja kwa wananchi  pamoja na mwekezaji ili kujadili...