Posts

Showing posts from December, 2022

RAIS DKT. SAMIA, WAZIRI MCHENGERWA WATUNUKIWA TUZO YA HESHIMA NA SHUKRAN TUZO ZA FILAMU 2022

Image
  Na John Mapepele Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mohamed Mchengerwa wametunukiwa Tuzo maalum ya shukrani kwa mchango wao katika kuleta mapinduzi makubwa kwenye sekta ya Sanaa. Tuzo hizo zimetolewa kwenye kilele cha utoaji wa Tuzo za Filamu 2022 uliofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye kituo cha Kimataifa cha Mkutano Arusha, AICC. Awali kabla ya kukabidhi Tuzo hizo, Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Filamu, Dkt. Kiagho Kilonzo amesema Mhe. Mchengerwa amechaguliwa kwa kuzingatia mchango wake mkubwa alioufanya katika kipindi kifupi tangu achaguliwe kusimamia sekta hiyo ambayo inaongoza kwenye kuchangia ukuaji wa uchumi. Amesema maelekezo ambayo amekuwa akiyatoa na kuyasimamia yamesaidia kukuza Sekta hiyo kwa kiwango kikubwa. "Ni kutokana na maelekezo thabiti ya Mheshimiwa Waziri ndiyo maana leo tunashuhudia kufanyika kwa mafanikio makubwa utoaji wa Tuzo wa msimu wa pili" amefafanua Kilonzo Tuzo ya Mhe. Rais ilikabidhi...

Mhe. Mchengerwa ahimiza kumuenzi Bibi Titi

Image
  Na John Mapepele Waziri Wa Utamaduni, Sanaa, Mhe. Mohamed Mchengerwa amehimiza umuhimu wa kumuenzi mwanaharakati  mwanamke, Bibi Titi Mohamed aliyefanya kazi kwa karibuni na Mwalimu Julisu Nyerere katika harakati za kuleta uhuru wa Tanganyika. Akizungumzia tamasha  la Bibi Titi Mohamed litakalofanyika  wilayani Rufiji, Mkoa wa Pwani, Mhe. Mchengerwa kwenye kipindi cha 360 cha kituo cha televisheni cha Clouds leo ambapo amesema  Bibi Titi ni alama ya mabadiliko katika suala zima la ushiriki wa wanakwake katika harakati hizo na kuleta mabadiliko.  “Ukimzungumzia Bibi Titi Mohamed unazungumzia alama ya mabadiliko, unazungumia alama ya kutoka kutoamini kuja katika kuamini kwa sababu Bibi Titi  mwenyewe aliamini kwamba tunaweza kujikomboa,” amesema. Amesema ni vigumu kuzungumzia mabadiliko ya kisiasa ya kuwaingiza wanawake katika siasa, ushawishi wa katika siasa, uchumi, matumizi ya Kiswahili,  bila kumzungumzia Bibi Titi Mohamed.   Amesema...